Zolla D akimbiwa Ulingoni
Mkali wa ngumi na muziki wa Hip Hop katika mitindo ya Mix Fighter David Michael Mlope, ama ukipenda unaweza kumwita King Zola D, hivi juzi amekimbiwa na mpinzani wake katika pambano lililoandaliwa na Kampuni ya Aulora, katika uwanja wa DDC mlimani Cyte.
Zolla amesema ingawa amepata ushindi wa Chee, lakini amehuzunika sana kwani amefanya mazoezi kwa muda mrefu akiwa na hamu ya kupigana, hatimaye mazoezi yote yamekuwa bule kwani mpizani wake ameingia mitini bila ya kuleta sababu za msingi.
Amesema huku ni kudumaa kwa ndundi kwa mtu kujitia woga usio wa msingi, kwani watu wametoa kiingilio kuja kuangalia ngumi sasa inakuwaje mtu ukimbie. Zola na Kiza kinene kama wangepigana ingekuwa ‘Game’ yao ya marudio kwani awamu ya kwanza walipigana mwishoni mwa mwaka 2009 kwenda 2010 na Kiza Kinene kupigwa vibaya na kuomba warudiane, lakini chaajabu leo hii wakati pambano limeshakamilika amekimbia wakati aliomba pambano kurudiana ni yeye.
Zolla D akiwa na Benjamini wa mambo Jambo wakiingia kwenye ukumbi wa DDC
Zola D akisalimiana na Ali Aurola(Wa pili kutoka mkono wa kulia)
Zolla D akiongea na simu, wakati akisubiri pambano
Zola D akiwa na mmoja wa makocha wake, wakisubiri pambano
Zola Akiwa na Kerven akimsubiri mpizani wake, ajitokeze jambo ambalo halikufua dafu, kwani mwenzake mapemba akilikuwa akila bata nyumbani.
Zola D akionyesha hisia zake kuudhunishwa kwa kutokuja kwa mpinzani wake.