Zola D na Mb Dogo kufunika Ujerumani 2012
Mkali wa muziki wa Hip Hop nchini Zola D, amesema kwa sasa ameungana na kampuni ya TIZO International, kwaajili ya kuusambaza mziki wa Bongo Fleva nchini Ujerumani. Mwanamuziki huyo amesema mpango mzima umesimamiwa na mwanadada
anayeishi nchini humo Tina Zobel, ambaye kwa pamoja wamepanga kuwa mapromota wa kuchukua wasanii ndani ya nchi na kupeleka nje, na pia kutoa wasanii nje ya nchi kuwaleta ndani.
Tina amesema kwamba lengo lao ni kuuwinua muziki huu nje na ndani ya Afrika. Zola amesema kwa sasa wanamikakati, ya kuanza safari yao ya kwanza, kwaajili ya kuandaa mazingira ya kufanya wasanii wengine wapite, kwakuwa yeye atakuwa tayari ameshasafisha njia ambayo wengine waje kupita, na kuweka mazingira mazuri ya tamasha yatakayofuatia baada ya yeye na Mb Dog.
Pia Tina ambaye raia wa Ujerumani lakini akiwa mzawa ‘Amezaliwa’ Kenya, amesema atafungua ofisi nchini Kenya na Tanzania, ambapo zitaanza kufanya kazi muda si mrefu, wakati Ujerumani tayari kampuni hiyo inafanya kazi.
Ratiba ya Zola na Mb Dog
Tina Zobel Impressum: TIZO International Promotions Keplerstrasse 8 74321 Bietigheim-Bissingen Germany |
||||||
|