Burudani
Zari akiri hadharani jinsi anavyompenda ‘mume’ wake Diamond
Mapenzi ya Diamond Platnumz na Zari The Boss Lady yanaonekana kuwa imara kadri siku zinavyokwenda, kutokana na jinsi mastaa hao wanavyozidi kuudhihirishia ulimwengu jinsi wanavyopendana.
Baada ya kumpata mtoto wao wa kwanza pamoja Princess Tiffah, couple hiyo imeendelea kushare na ulimwengu kupitia mitandao ya kijamii jinsi wanavyojiandaa kuja kuungana kuwa kitu kimoja hapo baadaye.
Licha ya kupost picha nyingi zinazodhihirisha upendo wao, Zari ambaye ni mama wa watato wanne hakusita kukiri hadharani jinsi anavyompenda Diamond ambaye humuita mume wake.
Kupitia Instagram alipost picha ya Diamond na kuandika;
“Have I ever told u how much I love this man. My hubby……”