Burudani

Young Killer: Hakuna msanii aliyenichomolea kufanya naye collabo

Ni kitambo sana kimepita tangu tumsikie rapper Young Killer kwenye collabo,hata Rremix pia ya Sinaga Swaga ameamua kufanya peke yake.

Wakati wengi tunahisi huenda ikawa wasanii wanachomoa kufanya ngoma na mkali huyo toka Rock City,mwenyewe amedai kuwa hakuna msanii yeyote ambaye alipanga kumshirikisha mwaka huu,akamtolea nje.

“Sijawahi kumtafuta msanii yoyote nifanye naye kazi kwa mwaka 2017 ambayo haijafanikiwa. Wote ambao niliwaapproach kufanya nao kazi,nimefanya nao kazi na zitatoka hivi karibuni,” amesema Young Killer.

Pia rapper huyo ameweka wazi kuwa muda si mrefu ataanza kutoa ngoma zake kupitia wasafi.com kwani tayari ameshasaini mkataba na platfoam hiyo mpya nchini.

By Prince Ramalove
Kings Fm

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents