Burudani

Young Killer azungumzia bajeti ya video ya ‘Umebadilika’, ‘nimeingia gharama kubwa’

Young Killer amesema ametumia gharama kubwa kufanikisha kushoot video ya wimbo wake ‘Umebadilika’ aliomshirikisha Banana Zorro.

KIller

Killer ameiambia Bongo5 kuwa zaidi ya shilingi milioni nane zimetumika hadi kuikamilisha. “Ni video ambayo nimeingia gharama kubwa, tofauti na video zote nilizowahi kuzifanya,” amesema rapper huyo. “Yaani ukianza kulinganisha video zangu ambazo zimepita nadhani kwa hii video inafikia katika maandalizi tu yaani sio hela ya kumlipa director ni kama milioni nne.”

Young Killer amesema ili kwenda kushoot video hiyo kisiwani Mbudya ilimlazimu kukodi boti kwa siku mbili.

“Hiyo ni kwenye mtumbwi tu, bado kuna ngalawa mle, tulikodisha ngalawa kushoot sehemu za Banana. Kuna watu waliocheza mle wamehitajika kulipwa, kuna majengo ya zamani tuliyakodisha, nauli za hapa na pale, watu wanahitaji wale,” ameongeza.

Rapper huyo amesema video hiyo ni kali kuliko hata anavyoisema mdomoni. “Naamini watakayoiona itakuwa kali zaidi ya hii ninayoisema.”

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents