Burudani
Young Dee amsaka kwa udi na uvumba mtu anayetapeli kwa jina lake Facebook, anataka amtupe ‘selo’
Rapper Young Dee amechoka na kutumiwa vibaya kwa jina lake kwenye mtandao wa Facebook na amedhamiria kumtupa selo mtu anayetumia jina lake kutapeli watu kwenye mtandao huo.
“Bado naendelea na zoezi langu, lakini sasa hivi nachokitafuta… kuna mtu wa sheria amenishauri kuna jinsi ambavyo hiyo kesi tunaweza kuifungua ikamake sense,” rapper huyo aliiambia website ya Times FM.
“Kwahiyo ndio niko naye naconfirm naye, lakini bado tunakusanya ushahidi. Kuna mtu mmoja nimempata ambaye ameshatapeliwa, natafuta mwingine. Kwa hiyo tukishapata ushahidi wa kutosha tunaweza kum-sue.”