Yaliyomkuta Temba video ya bibi Cheka
Mwanamuziki kutoka pande za Kiumeni Temeke Amani Temba maarufu kama Mh Temba, yule mkali wa kukata mapanga katika kundi la Tmk Wanume Family chini ya kiongozi Saidi Fella, jana amejikuta akiingia kwenye masahibu makubwa ya kutapika baada ya kukutana na damu ya mtu Live, wakati akifanya video ya mwanamuziki mwenye umri mkubwa kuliko wote katika muziki wa Bongo Fleva, Bibi Cheka.Mkali huyo ambaye alitoka Jeshini na kuangukia kwenye Bongo Fleva, alikuwa ni msanii aliyeshirikishwa kwenye wimbo huo unaoitwa Ni wewe, ndipo moja ya Clip, ilimtaka Temba awe majeruhi na kisha kuingizwa kwenye Ambulance ambapo humo ndani atakuwa akiangusha mistari bin michano ya wimbo huo. lakini hatmaye mwanamuziki huyo alishindwa kufanya chochote na kujikuta akitapika hasa baada ya kukutana na damu ya mtu .Picha lilianza hivi….