Burudani

Wolper awajia juu wanaofuatilia penzi lake jipya na Harmonize

Jacqueline Wolper amewafungukia wanaomsema kuwa haendani na mpenzi wake mpya, Harmonize.

c79e987f-01b7-4137-abf1-e66acf4f90cf

Hivi karibuni familia ya WCB imeonekana kuchafua hali ya hewa mitandaoni baada ya picha zilizokuwa zinasambaa zikionyesha couple hiyo mpya mjini kati ya Jacqueline Wolper na Harmonize huku baadhi ya mashabiki wakisema kuwa ilikuwa ni kiki lakini kwa sasa mambo yanaonekana kubadilika.

Akiongea kwenye kipindi cha Take One, kinachoruka kupitia Clouds TV, Wolper alisema kuwa anaweza akawa na mwanaume anayefanya kazi yeyote sababu haitaji pesa kutoka kwa mwanaume.

“Naweza hata nikawa na mtu anaendesha bodaboda au anaweza sijua akawa mfagia hoteli, sijui anafagia nini lakini mimi kama mimi nikambadilisha na akawa mwanaume wangu. Kwa sababu nachokihitaji mimi sihitaji pesa mimi ni mpiga kazi, mimi nafanya kazi na ndiyo maana mwanzo nimeanza like na fanya promosheni Napata hela yangu, sitaki kutegemea mtu,” aliongeza.

Wolper alianzisha uhusiano na muimbaji huyo wa ‘Bado’ baada ya kuvunja uchumba na mwanaume aliyeahidi kumsomesha nchini Afrika Kusini na ambaye alikuja kugundua kuwa ni mume wa mtu.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents