Burudani

Wolper aeleza yaliyomkuta mpaka akampiga chini Mkongo, adai Mkongo alimpiga picha za uchi ili asimuache

Msanii wa filamu Jacqueline Wolper amefunguka na kuzungumzia sababu ya kuachana na aliyekuwa mpenzi wake ambaye alimvalisha pete ya uchumba pamoja na kwenda kwao kwa ajili ya maandalizi ya kumtolea mahari ili amuoe.
wolp2
Wopler na mpenzi wake wa zamani

Muigizaji huyo ambaye amekiri kutoka kimapenzi na Harmonize wa WCB, amekiambia kipindi cha Take One cha Clouds TV kuwa, Mkongo huyo ambaye alimvalisha pete ya uchumba, alikuwa ana mke pamoja na mtoto na pia alimfanyia kitendo cha kinyama cha kumrekodi picha za uchi ili asimuche.

“Mimemvumilia kumkuta na picha zangu za uchi, video zangu za uchi,” alisema Wopler huku akilia.

“Nikiongelea nimezionaje nitakuwa namvunjia heshima, kwa sababu kuna kitu kibaya alikifanya. Kuna matatizo ambayo yalitokea nikawa namkwepa, niligundua ana matatizo mengi nikawa namkwepa, nilikuwa na stress nikawa nalewa sana, nalewa mpaka nazima. Sasa siku ambayo nimelewa sana mpaka nimezima akaambiwa nilipo, nilikuwa nipo mimi, dada yangu mmoja pamoja na mdogo wangu mmoja nimelewa chakari, nimechanyikiwa siyo mimi. So kilichotokea akaja akanichukua, akanipeleka nyumbani kwake, akanivua nguo zote, nilikaa kwenye kitanda chake, nipo uchi wa mnyama, yaani sijui chochote kinachofanyika, akarekodi video na kunipiga picha,” aliongeza Wolper.

c79e987f-01b7-4137-abf1-e66acf4f90cf
Harmonize na Wopler ndani ya mahaba

Muigizaji huyo amesema baada ya kugundua kuwa mpenzi wake huyo alimpiga picha za uchi, alimuomba azifute lakini akawa anamtishia kuzisambaza kama akimuacha.

“Kitu cha ajabu ambacho kilikuja kunishangaza wiki mbili zilizopita, aliniambia kitu nitachokifanya baada ya kugundua kwake sipo vile kama zamani, akaniambia kitu nitakacho kufanya, watanzania watafunga macho, meseji zake zote ninazo na nimemkabidhi mwanasheria wangu na nimeshaandikisha kila kitu, akaniambia kitu nitakacho kifanya watanzania hawata amini, nikamwambia najua ulinichua video za uchi, akaniambia kumbe ndiyo hicho tu unachokifahamu, sasa sijajua ni nini sijawahi kufanya uhalifu kwake wala nini,” alisema Wolper.

Pia Wolper amedai alipelekwa Afrika Kusini ili akasome lakini akaishia kudanganywa na kukaa Afrika Kusini kwa miezi mitatu bila chochote na kuamua kurudi zake Dar es salaam.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents