Wizkid na Victoria Kimani washoot video Kenya na Enos Olik
Staa wa Nigeria Wizkid amekuwepo Afrika Mashariki kwa takribani wiki moja. Alianzia jijini Nairobi Kenya ambapo Jumapili iliyopita alitumbuiza kwenye viwanja vya The Carnivore, na baadae kuelekea jijini Kampala Uganda ambako alitumbuiza kwenye Party ya Guiness na kisha akarudi tena Kenya ambako imefahamika alirudi kushoot video.
Victoria Kimani (kushoto) Wizkid (Kulia)
Staa huyo wa ‘If I Show You My Money’ ameshoot video nchini Kenya na director Mkenya Enos Olik ambaye amewahi kufanya video za wasanii wa Bongo kama Weusi (Gere), Vanessa Mdee (Come Over) na video mpya ya Shaa (Njoo).
Wizkid ameshare picha Instagram akiwa na Victoria Kimani na kuandika:
“Videoshoot in Kenya!! Big up @iamdelb @victoriakimani nd @patrickelis !! Thank u Nairobi u have been good to us. We off!”
Director Enos Olik amethibitisha juu ya uchukuaji wa video ya Wizkid kwa kushare picha akiwa nae na kuandika:
“Me and my bro @wizkidayo About to kill it on Set…#MusicVideoTings
#Kenya #Naija #Connection . #BokehFamily “
Victoria Kimani ambaye pia anaonekana kuhusika kwenye video hiyo nae ameshare picha na kuandika:
“Video shoot fresh @wizkidayo”