Burudani
Witness (rapper): Sijawahi kupewa heshima ninayostahili Tanzania
Rapper Witness amesema pamoja na kuwa na mchango mkubwa kwenye muziki wa hip hop Tanzania, hajawahi kupewa heshima anayostahili.
Witness ameiambia Bongo5 kuwa kitendo hicho kimekuwa kikimvunja moyo.
“Mimi ni msanii pekee wa kike wa hip hop nchini Tanzania ambaye bado nipo na ambaye huwa anawakilisha watanzania, either wa kike au wa kiume kwenye hip hop industry hata kwa nje ya nchi,” amesema. “Kitu kinachonisikitisha ni kwamba sijawahi kuwa recognized hata siku moja hata tu kwenye radio station ama TV station ama kwenye hizi awards.”
Rapper huyo amesema hiyo ni moja ya sababu zinazowakatisha tamaa wasanii wa hip hop wa kike nchini.Msikilize zaidi hapo chini.