Burudani

Wimbo ambao natamani kuandikia script ya video ni ‘Zigo’ ya AY – Asema Mike Tee

Mike Francis Mwakatundu maarufu kama Mike Tee, ni rapper mkongwe kutoka Iringa ambaye pia ana uwezo mwingine wa kuandaa ‘script’ za video za muziki.

mike-tee

Mike Tee ndiye aliandika script ya video ya Mwana FA na Alikiba ‘Kiboko Yangu’ iliyoongozwa na director Mkenya, Kevin Bosco.

Kupitia 255 ya XXL Mike amesema wimbo anaotamani kuandikia script ya video kwa sasa ni ‘Zigo’ ya AY.

“Nyimbo moja ambayo napenda sana yaani nikiiskiliza inaninivutia sasa hivi na ningepedna sana kuichorea script ni ‘Zigo’ ya AY” amesema Mike Tee.

“kwenye nyimbo ya Zigo amenifurahisha sana Ile nyimbo kila nikiiskiliza naiangalia ina mazingira ya aina tatu kwasababu nyimbo yenyewe imegawanyika mara tatu, kwahiyo napenda kuchora nioneshe mazingira halisi ya Tanzania yaani tunataka kitu kizuri lakini kwa location za Tanzania.” Alisema Mike Tee.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents