Burudani

Weusi kuzindua video zao 5 mpya kwenye show ya ‘Funga mwaka la Weusi’ Jumamosi hii Dar

Familia ya Weusi inaendelea kuonesha matunda ya muungano wao, wakiwa wanaendelea na ziara ya show zao za Funga mwaka, wiki hii Weusi wanatarajia kuzindua video zao tano kwa mpigo pale Escape One, jijini Dar es salaam.

weusi gere

Msemaji wa kundi hilo Nikki Wa Pili amezitaja video watakazozindua Jumamosi hii November 29, kuwa ni video yake ya ‘Sitaki Kazi’ iliyofanywa Arusha na director Mkenya Enos Olik. Video ya ‘I See Me’ ya Joh Makini iliyofaywa Nairobi na Olik, Video ya ‘Mavijanaa’ ya G-Nako iliyofanywa Arusha na Olik.

Nyingine ni video ya Joh Makini ‘XO’ iliyofanywa na Nisher , pamoja na video nyingine ya G-Nako inaitwa ‘Morale’ imefanywa na Halfani.

“Zote tano tutazizindua Jumamosi Escape One katika Funga mwaka la weusi jijini Dar es salaam.Sio mchezo si unajua game linabadilika kwahiyo formula na zenyewe zinabadilika kila siku.” Nikki ameiambia 255 ya XXL ya Clouds Fm.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents