Michezo

West ham wampa mkataba mpya mchezaji Dimitri Payet

Kiungo mshambuliaji wa timu ya taifa Ufaransa na klabu ya West ham, Dimitri Payet amesani tena mkataba mpya wa miaka mitano na timu yake hiyo.
Payet mwenye umri wa 28 alijiunga na West ham ya Jijini London msimu uliopita akitokea timu Marseille kwa dau la zaidi ya pauni milioni 10.

311A8D2C00000578-3442914-Payet_is_all_smiles_as_he_agrees_his_new_deal_with_Premier_Leagu-a-21_1455222032377

Wiki hii klabu yake ilizikataa taarifa zilizosambaa kuwa mchezaji huyo anataka mkataba mpya, huku mkataba wake wa kwanza pia ukiwa ni miaka mitano.

Mchezaji huyu kutoka Ufaransa amefunga mara 6 katika michezo 22 aliyocheza na kuiweka West Ham katika nafasi ya sita ya msimamo wa ligi kuu ya England.
David Sullivan, mmiliki wa timu hiyo amesema “tutafanya chochote kuwabakiwa wachezaji wetu wazuri na Payet ni mchezaji mzuri.”

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents