Michezo

Waziri Nape aufungua tena uwanja wa taifa kwa mechi za ligi kuu

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia kwa Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Nape Nnauye wametangaza kuufungua tena uwanja wa taifa baada ya kuufunga mwezi Oktoba mwaka jana kwa shughuli zozote.

Uwanja huo ulifungwa kutokana na uharibifu uliotokea wakati wa vurugu zilizotokea uwanja huo wakati wa mechi ya watani wa jadi Simba na Yanga iliyochezwa Oktoba 1 mwaka jana. Uwanja huo utaanza kutumika katika mechi ya Simba na Azam itakayochezwa Jumamosi hii.

Soma taarifa hiyo zaidi hapa chini.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents