Habari

Waziri Nape atema cheche kwa wasanii wasiomuunga mkono kupambana na wizi wa kazi za wasanii

Waziri wa Habari, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye amewataka wasanii nchini kumuunga mkono katika jitihada zake za kupambana na wezi wa kazi za wasanii kuliko kuendelea kutoa siri za mapambano yake kwa wahusika wanaowanyonya wasanii huku akidai wasanii wakubwa wa sekta hiyo hawampi ushirikiano.

Waziri Nape ameyasema hayo jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na wadau wa sanaa mbalimbali akieleza baadhi ya wasanii wakubwa wapo lakini hawatoi ushirikiano wowowte ili hata pale wanapotakiwa kusaidiana na wizara kupambana na wezi wa kazi za sekta hiyo.

“Nilisema kwenye operesheni hii tuambatane na watu ambao wanafanya kazi hii, ili waunge mkono kwasababu hii inatakiwa kuwa kama kampeni tukawaline up wasanii wote wakubwa walikimbia, wewe unajua, wote walikimbia,” alisisitiza Nape.

“Hata nyinyi wasambazaji wa kazi za ndani sikumuona hata mmoja, unajua waziri umeenda umefanya operesheni umemaliza mimi nilitegemea nyinyi mnakaa mnawaita wana habari mnasema tunamuunga mkono waziri na tutasimama nae kuhakikisha hili jambo linafanikiwa, lakini wote walikimbia”.

BY: Emmy Mwaipopo

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents