Picha
Watu wawili waliokuwa wakishikilia mateka kanisani wauawa Ufaransa
Watu wawili waliokuwa na silaha na waliokuwa wameshikilia mateka kwenye kanisa moja huko Rouen, Kaskazini mwa Ufaransa wameuwa.
Mateka mmoja pia ameuawa. Watu hao walikuwa wakishikilia mateka watu wanne hadi sita kwenye kanisa la Saint-Etienne-du-Rouvray.
Padre, watawa wawili na waumini walikuwa miongoni mwa watu waliokuwa wameshikiliwa. Polisi wamelizunguka kanisa hilo na watu wameambiwa kukaa mbali.