Habari
Watanzania waanzisha mtandao wa kijamii na kiuchumi, ‘Mambopoint’
Mtandao wa kijamii na kiuchumi uitwao mambopoint.com umeanziswa na watanzania ukiwa na lengo la kuimarisha usalama wa matumizi ya mitandao ya kijamii nchini.
Mbali na kufurahia huduma za kupost picha, kupeana comment na Admires (likes) ku-update status na live chatting mambopoint.com imezingatia mahitaji ya vijana wa kitanzania ambao wengi wanatafuta ajira hivyo kutoa huduma ya kuona matangazo mbalimbali ya kazi zinazotangazwa kila siku.
Ukiangia kwenye anuani ya mtandao huo upande wa kushoto kunaonekana link mbalimbali kama vile Job, find friend, career na vingine ili kumwezesha mtumiaji kutumia mtandao huo kwa urahisi zaidi.