Wataalam: Internet yaanza kujaa, makampuni yapata hasara baada ya kupotea hewani kutokana na ufinyu wa nafasi mtandaoni
Wataalam wameonya kuwa kuna uwezekano tatizo la mitandao mingi kupotea hewani mara kwa mara likawa la kawaida hapo mbeleni kutokana na hofu ya kuwa ‘internet’ inaelekea kujaa. Inadaiwa kuwa hofu hiyo inatokana na matumizi ya ‘internet’ kuzidi kiwango cha juu.
Jumanne wiki hii (Agosti 12) makampuni mbalimbali makubwa duniani yanayotegemea zaidi mtandao wa ‘internet’ katika uendeshaji wa shughuli zao, yalipata hasara kufuatia kupotea kwa mawasiliano ya ‘internet’ kwa muda mrefu.
Miongoni mwa makampuni yaliyoathirika ni pamoja na eBay, ambao ni mtandao wa kuuza na kununua bidhaa mtandaoni, baada ya internet kupotea hewani kwa takriban siku nzima na kusababisha baadhi ya wateja kudai warejeshewe fedha zao walizonunulia bidhaa.
Inaelezwa kuwa tatizo kama lililotokea Jumanne lilitokana na kitu kinachofahamika kama ‘Boarder Gateway Protocal’ (BGP).
“The problem is understood to have been caused by the crucial ‘nuts and bolts’ of the internet – called the Border Gateway Protocol (BGP).” Uliandika mtandao wa Daily Mail.
“Internet companies and large networks use this ‘route map’ – consisting of hundreds of thousands of complex paths through the web – to send information to each other.
When visiting a website, users rely on machines called routers to remember how to navigate trusted routes through the ever-expanding internet.”
Tazama video inayoelezea kuhusu BGP na inavyofanya kazi
Isome zaidi habari hiyo hapa.
Source: Daily Mail