Wasanii wengi sasa hivi wako ‘too shallow’ – Jay Moe (Audio)
Rapper Jay Moe amesema wasanii wa sasa wengi wako ‘too shallow.’
Moe amesema hayo kwenye mahojiano na mtangazaji wa Jembe FM, JJ.
“Anaweza akawa anajua kurap, lakini kwenye verse ya kitu anachokirap kwa mtu mwenye uelewa na kwa mtu mfuatiliaji wa vitu vingi ya dunia ya sasa hivi unaweza usirelate na leo ni sababu wasanii wengi wa sasa hivi atasikia tu neno tumbua majipu kesho unashangaa kuna wimbo unaitwa hivyo. Wimbo unaitwa Mwendo Kasi, no disrespect kwa mtu yeyote mwenye wimbo unaitwa jina hilo lakini kwangu mimi naona hakuna ubunifu mwingi zaidi ya neno fulani linatamba mjini basi analitumia,” amesisitiza.
“Wasanii wa sasa wanafocus zaidi kwenye Snapchat, Instagram kupost mapicha kuliko kwenye Wikipedia, google na kufanya tafiti ya kiti fulani. Hawana reference kwenye nyimbo zao.”
Msikilize zaidi hapo chini.