Wasanii wa komedi kuungana na familia ya Sharo Milionea kufanya dua
Wasanii wa filamu za vichekesho nchini leo wataungana na familia ya marehemu Sharo Milionea kufanya dua. Leo ni mwaka wa pili tangu msanii huyo afariki kwa ajali ya gari.
Akizungumza na Bongo5 leo, Kitale aliyekuwa rafiki wa karibu wa msanii huyo alisema wasanii wa komedi wameona kuna kila sababu ya kwenda nyumbani kwa marehemu na kufanya dua hiyo.
“Unajua sisi ni wasanii ambao tulikuwa karibu na Sharo, sasa tukaona kwanini tusisafiri na kwenda Tanga kujumuika na wana ndugu wa Sharo na kufanya dua maalum kwaajili ya kumkumbuka mwenzetu! Hakuna kitu kikubwa zaidi ambacho tunaweza kukifanya kwaajili ya marehemu zaidi ya dua. Kwahiyo leo ndo safari ya kwenda Tanga na kufanya dua hiyo ambayo itahudhuriwa na wasanii mbalimbali wa komedi,” alisema Kitale.