Wasanii wa filamu na Bongo fleva waupamba uzinduzi wa Zuku Tv
Wasanii mbalimbali jana walikusanyika katika uzinduzi wa stesheni ya tv ya Zuku Tv katika Hoteli ya Golden Tulip, sherehe hiyo iliudhuriwa na wajumbe mbalimbali wa sector ya mawasiliano walishiriki pamoja na watu mbalimbali waliokuja kushuhudia uzinduzi huo.
(Anti Ezekiel akiwa na Monalisa katika moja ya pozi katika uzinduzi wa Zuku Tv pale Golden Tulip)
Mwenyekiti wa wa Mwananchi Group Bw Ali Mufukuru, aliizindua Zuku Tv kwa kubonyeza remonti na televisheni zote zilizopo hapo ukumbini kuonyesha vipindi mbalimbali vya Zuku ikifuatiwa na maonyesho ya Fataki.
(Kweli mpiga picha naye hupigwa, Bukuku akiwa anarainisha koo, wakati wa uzinduzi wa Zuku Tv.)
Televisheni ya Zuku itakuwa inatoa uchaguzi mpana wa stesheni za burudani ikiwa ni pamoja na habari, Michezo na sinema, majarida na muziki. Hivi vinajumuisha chaneli za nje, kama vile BBC, MTV Base,Sentanta Sports, MGM Movies na zingine.
( Mkali wa Afrika mashariki na kati katika staili mzima ya uimbaji wa Twista, Abwene Yesaya aliyevaa kofia nyeusi akiwa na rafiki zake, katika uzinduzi wa Zuku Tv)
Msambazaji atatoa hofa kabambe za stesheni kama vile Zuku Afrika, ambayo huonyesha bara la Afrika, Zuku Life, ambayo huonyesha Docomentari mbalimbali, Zuku Sports pamoja na Chaneli kibao za Sinema. Huduma hii ya Zuku Tv itapatikana kupitia Satelait Tanzania nzima
Cloud 112, akiwa kwenye pozi na kimwana wa Bongo Movie
Ngosha ama Fid Q akiwa na mwana Fa kwenye pozi wakisubiri zamu yao ya kupanda jukwaani katika uzinduzi wa Zuku Tv
Mwigizaji wa filamu akiwa ametulia na mwigizaji mwenzake mwenye mvuto wa kipeee Ant Ezekiel.
Linex akijiachia na wasanii wenzake
Mkubwa na wanawe, akiongozwa na meneja wao Yusuph, Aslay, Mr India na Mohamedi katika pozi
Mama yake na Monalisa, Natasha
Roma mkatoliki, akikamua wakati wa tamasha la uzinduzi wa Zuku Tv