Burudani

Wasanii 10 wapya Tanzania wa kuwaangalia mwaka 2013

Ally Nipishe

Zikiwa zimebaki siku chache tu mpaka tuumalize mwaka 2012, Bongo5 imewaangalia wasanii 10 wapya wa Tanzania ambao huenda mwaka 2013 ukawa wao. Hii ndio list ya wasanii hao.

1. Ally Nipishe

Ally kwenye picha hapo juu ni kijana aliyeupendezesha wimbo wa Mwasiti, ‘Mapito’, ambao ni miongoni mwa nyimbo zilizofanya vizuri zaidi mwaka 2013. Kijana huyu kutoka THT, ni tishio kubwa kwa wasanii wenye uimbaji kama yeye ambao ni pamoja na Barnaba, Amini na wengine. Kwa sasa ana wimbo wake mwenyewe uitwao My.

2. Vanessa Mdee

Vanessa Mdee

Mtangazaji huyu wa MTV Base na Choice FM ameonesha uwezo mkubwa katika kuimba mwaka huu baada ya kushirikishwa kwenye wimbo Money wa AY na Me and You alioshirikishwa na Ommy Dimpoz. Me and You unafanya vizuri kwenye radio za Afrika Mashariki na ndio uliodhihirisha uwezo mkubwa wa uimbaji aliojaaliwa mrembo huyu. Hivi karibuni, Vanessa ameonesha uwezo mwingine wa kurap katika wimbo alioshirikishwa na Dj Choka, Press Play. Watu wengi wanausubiri ujio wake mwenyewe.

3. Walter Chilambo

Walter

Mshindi huyu wa kitita cha shilingi milioni 50 za Bongo Star Search 2012 mwenye mashabiki lukuki nchini ameonesha kila dalili ya kuiondoa aibu ya washindi waliopita wa shindano hilo ambao wameshindwa kufanya vizuri sokoni. Sauti ya pekee aliyonayo Walter inaashiria kuwa mwaka 2013 utakuwa wake pia.

4. Mirror

Mirror (Kulia)
Mirror (Kulia)

Ni msanii mwenye sauti ya aina yake kabisa. Ukiusikia wimbo wake ukichezwa redioni ni lazima upate shauku ya kumfahamu. Ana video moja hewani ya wimbo wake uliotengenezwa na Manecky ambao unatoa kila sababu za kijana huyu kufanya vizuri mwakani.

5. Cliff Mitindo

Cliff Mitindo

Cliff ni rapper mwenye uwezo mkubwa wa Freestyle. Alifanya vizuri kwenye cypher ya Fiesta 2012 iliyowakutanisha mastaa kibao wakiwemo Godzilla, Fid Q, Babuu wa Kitaa, Nikki wa Pili, Stamina na wengine. Ana ngoma yake mpya iitwayo Ha ha ha ambayo inafanya vizuri redioni na kuuonesha upekee wake katika uandikaji na uwasilishaji wa michano.

6. M-Rap

M-Rap (kulia) akiwa na Pancho
M-Rap (kulia) akiwa na Pancho

M-Rap ni rapper aliye kidato cha sita ambaye yupo chini ya label ya B’Hits. Ana wimbo wake uitwao Destiny ambao licha ya kuwa na sauti ya utoto, M-Rap ni rapper mwenye uwezo mkubwa wa kiuandishi. Unaweza kumsikia pia kwenye Press Play ya Dj Choka ambapo ameimba verse ya kwanza.

7. Kankaraga

kankaraga

Hili ni kundi la wasanii watatu wa kike kutoka THT. Akina dada hawa utawapenda ukiwaona kwenye stage wakiperform. Wakiwa na kila sifa za kuwa madansa, Kankaraga wamedhihirisha uwezo mwingine mkubwa wa kuimba hasa kama ukisikiliza wimbo wao wa kwanza, ‘Kankaraga’. Mwaka 2013 bila shaka umewawekea nafasi yao.

8. Young Killa

Young Killa aliyevua shati
Young Killa aliyevua shati

Kijana huyu kutoka Mwanza ni miongoni mwa wasanii wachanga waliopewa salute na Fareed Kubanda aka Fid Q. Wajua Fid akimkubali mtu. Young Killa alikuwa miongoni mwa washindi wa Super Nyota ya Fiesta na alifanikiwa kuzunguka mikoa yote Fiesta ilikofanyika mwaka huu. Uandishi wa nyimbo zake una uelekeo wa wasanii kama One The Incredible, Nikki Mbishi na Stereo.

9. Vida

vida

Kama umewahi kuusikia wimbo uitwao ‘Baba Awena’ utakuwa umemsikia dada mmoja mwenye sauti tamu iwezayo kumtoa nyoka pangoni. Huyo ni Vida zao jingine kutoka TH. Katika wimbo huo Vida amemshirikisha Linex.

10. Kadgo

Kadgo (kushoto) akiwa na Fid
Kadgo (kushoto) akiwa na Fid

Kadgo ni mwakilishi mwingine wa Rock City ambaye yeye pamoja na Young Killa wapo chini ya uangalizi mzuri pia wa Fid. Kadgo kwa sasa ni msanii aliye chini ya Tamaduni Muzik na M-Lab. Uwezo wake katika kuandika mashairi yenye mistari konde isiyo na idadi si wa kifani.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents