Burudani

Walter Chilambo ataja mabadiliko aliyoyaona tangu alipoingia kwenye muziki wa injili

Walter Chilambo amefunguka mabadiliko aliyonayo kwa sasa tangu alipotangaza kuingia katika tasnia ya muziki wa injili.

Kupitia kipindi cha V-Mix cha Channel 10 cha Mwaka The Boy, Walter amesema, “Nimebadilika vingi japo kama mwanadamu kimuonekano bado nipo vile vile lakini ndani yangu nimebadilika vingi sana. Nimekuwa na amani zaidi na nimekuwa najua nipo huru zaidi tofauti na nilivyokuwa mwanzo.”

“Sijawahi kuona Bongo Fleva ngumu na wala sijawahi kuona ugumu wowote kwangu na kama ingekuwa ngumu nisingekuwa na mafanikio ambayo tayari nilikuwa nimeyapata,” ameongeza.

Mpaka sasa Walter ameshaachia nyimbo mbili za muziki wa injili ikiwemo ‘Asante’ na ‘Merry Christmas’ tangu alipotangaza rasmi mwaka mwishoni kuingia kwenye muziki huo.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents