Mitindo

Wabunifu chipukizi wapatikana

 

Wabunifu 8 wenye vipaji  wameingia katika fainali  za kushindania zawadi za maonyesho makubwa ya mavazi ya Swahili Fashion Week 2010 wamepatikana.

Uchaguzi huo wa wabunifu wa mavazi wanaochipukia ulifanyika Jumapili  katika Hoteli ya Southern Sun Hoteli jijini Dar es Salaam, ambapo majina 8 yaliteuliwa na jopo la majaji wanne  ambao  ni Nsao ShaluA, Mkurugenzi wa sanaa kutoka baraza la sanaa la Taifa (National arts Council), Jamila Swai, mbunifu wa mavazi wa hapa nchini, Michelangelo Adam kutoka Ubalozi wa Italia hapa nchini pamoja na Mustafa Hassanali, kati ya waratibu wa Swahili Fashion Week 2010.

Wabunifu hao waliobahatika kuingia fainali, watashindana kwa kuonyesha kazi zao katika maonyesho makubwa ya wiki ya mavazi ya Swahili fashion week  itakayofanyika Novemba mwaka huu.

Wabunifu wa mavazi wanaochipukia waliofanikiwa kuingia fainali ni pamoja na Narendrakumar Jeshang, Abdul Urassa, Shaban Wahure, Angelina Muna  na Grace Kijo.
Awali mratibu wa Swahili Fashion Week,Washingtone Benbella alisema kuwa wabunifu wote 16 walikuwa wazuri na wameonyesha vipaji vya hali ya juu, na kuonyesha kuwa Tanzani ina vipaji vikubwa katika sanaa ya ubunifu wa mavazi.

Ni mara ya tatu tangu Swahili fashion week kuanzishwa na inatarajiwa kufanyika  tena Novemba  mwaka huu jijini Dar es Salaam.

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents