Promotion

Vodacom: Kuweni macho na matapeli wa fedha za M-Pesa

Ikiwa wateja mbalimbali wa Vodacom Tanzania wakiendelea kunufaika na bonasi za M-PESA zinazotolewa na kampuni hiyo, kumetokea na matapeli wakiwalaghai wateja wa kampuni hiyo kana kwamba ni washindi wa bonasi hizo zinazoendelea kutolewa.

Vodacom Tanzania imetoa tahadhari kwa wateja wake wote popote walipo nchini kuwa macho na matapeli ambao wanajifanya ni wafanyakazi wa kampuni hiyo kwa kuwapigia simu na kuwafahamisha kuwa wamefanikiwa kupata mgao wa fedha za gawio la huduma ya M-Pesa uliotangazwa na kampuni mapema wiki hii.

Akiongea na Mtandao huu,Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania, Jacqueline Materu alisema, “Natoa wito kwa wateja wetu kuwa makini na matapeli wanaowapigia simu na kuwafahamisha kuwa wameshinda fedha za bonasi ya M-Pesa.Vodacom Tanzania haina utaratibu wa kuwapigia simu wateja kuhusiana na mgao wa fedha hizi bali inatoa mgao kwa kadri ya mteja alivyotumia huduma hii na rekodi zote za matumizi kampuni inazo. Wanaowapigia simu wateja ni matapeli ambao wanataka kupata namba zenu za siri na kuwatajia kiasi gani cha fedha mlizonazo ili wapate frusa ya kuwaibia fedha na msitoe namba za siri kwa mtu yeyote.”.

Wateja watakaonufaika na mgao wa fedha za bonasi ya M-pesa awamu hii wanawekewa fedha zao kwenye akaunti zao za M-Pesa moja kwa moja na utaratibu wa kuwapigia wateja simu huwa unatumika kwenye promosheni tu kama vile promosheni inayoendelea ya”Nogesha Upendo”.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents