Vodacom kuongeza udhamini wa Miss Tanzania
Jana jioni Vodacom wametangaza kuongeza mkataba wa kudhamini mashindano
ya Miss Tanzania kwa muda wa miaka miwili. Waliyoangusha wino katika
mkataba huu ni Hashim Lundenga mkurugenzi kamati ya Miss Tanzania, na
George Rwehumbiza Meneja Udhamini na Mawasiliano Vodacom.
Nia ya Vodacom ni kuboresha zaidi mashindano, mwaka jana Vodacom ilidhamini kwa zaidi ya shilingi miloni 600.
Mkurugenzi wa Kamati ya Miss Tanzania Hashim Lundenga kulia na Meneja udhamini na mawasiliano wa Vodacom George Rwehumbiza walibadilishana mikataba ya udhamini wa shindano hilo mara baada ya kasaini mbele ya waandishi wa habari na wageni mbalimbali walioalikwa katika uzinduzi huo, iliyofanyika katika hotely ya Regency Park Hotel.