Video ya msanii wa Diamond, Harmonize yashootiwa Afrika Kusini na imekamilika
Msanii anayesimamiwa na Diamond Platnumz kupitia label yake WCB, Hamonize anaendelea kuziona faida za kuwa chini ya msanii mkubwa mwenye connections nyingi.
Harmonize licha ya kuwa ni msanii mpya lakini safari yake ya kimuziki imeanzia kwenye matawi ya juu ambayo kuna baadhi ya wasanii wakubwa hawajawahi kuyafikia.
Harmonize amesema kuwa video ya single yake ya kwanza ‘Aiyola’ tayari imekamilika, ikiwa imeshootiwa Afrika Kusini na director aliyeongoza video ya mastaa wa Nigeria, ‘Dorro bucci’ pamoja na ‘Love Boat’ ya Kcee na Diamond.
Kupitia Planet Bongo ya EA Radio, Harmonize ameongeza kuwa tayari amewasiliana na director na amemtumia video hiyo ikiwa imekamilika.
Sina shaka siku si nyingi tutaanza kumuona Harmonize akisumbua kwenye vituo mbalimbali vya kimataifa kama Trace na MTV Base ambavyo vimekuwa ni ndoto za wasanii wengi wa Bongo.