Burudani
Video: Siku mchekeshaji Anne Kansiime wa Uganda alipoamua kuimba!
Wiki iliyopita mchekeshaji wa kike kutoka Uganda, Anne Kansiime alishika nafasi ya kwanza katika orodha ya watu 100 maarufu wa Uganda, ‘Uganda’s top 100 celebrities’. Kikubwa zaidi hadi kufanya mitandao mingine iandike habari hiyo kwa kuanza na neno ‘Shocking’, ni kwasababu Kansiime alimzidi hata mwimbaji Jose Chameleone, aliyekamata nafasi ya nne kwenye orodha hiyo iliyoandaliwa na New Vision ya Uganda.
Cheka na ufurahi kwa kutazama sehemu ndogo ya uchekeshaji wa Kansiime ambaye hapa aliamua kuimba, tena kwa hisia.