Rapper wa Tanzania, Kiche Legend ameiwakilisha Tanzania kwenye mradi wa Next Level nchini Marekani.
Next Level ni mradi wa wizara ya mambo ya nje ya Marekan na chuo kikuu cha North Carolina kupitia idara yake ya muziki inayosaidia kukuza mabadilishano ya kimataifa ya utamaduni na usuluhishi wa migogoro kupitia hip hop na kucheza.
“Napenda nchi yangu, Napenda watu wangu, Napenda Muziki, Napenda Hip hop #reppin #255 #Tz #nextlevelusa #hiphop #hiphopdiplomacy #leader #NewLegends #TeamMBWIGA,” ameandika Kiche kwenye Instagram.
Kiche ameungana na rappers wengine kutoka Serbia, Senegal, na Thailand.