Burudani

Video: Rapper wa Marekani avunja mahojiano baada ya kuguswa na Beyonce

Hata ukiwa unajiona wewe ni muongeaji sana lakini siyo pale utakapokutana na Beyonce – unaweza ukageuka bubu kwa muda.

chance-the-rapper-beyonce-vmas-backstage

Kilichomtokea rapper wa Chicago, Chance the Rapper wikiendi hii kwenye backstage ya tuzo za MTV VMA lazima atakiweka kwenye kumbukumbu ya maisha yake kwa kuwa watu wengi wanatamani kiwatokee.

Wakati Chance the Rapper akihojiwa na mtangazaji wa MTV, Meredith Graves kuna mtu alikuja nyuma ya rapper huyo na kumlalia kwenye upande wa bega lake la kushoto alipogeuka alishangaa kumuona ni Beyonce aliyefanya kitendo hicho.

Ilikuwa ni kama ndoto kwa rapper huyo alijikuta akimkumbatia malkia huyo na kushindwa kumwambia chochote na hata interview ikaishia hapo huku akimalizia kwa kusema “This is my life.”

Hata Dj Khaled aliwahi kuliambia gazeti la The New York Times kuwa heshima aliyonayo kwa Bey ni kubwa mno kiasi cha kuwa muoga wa kuongea sana akiwa naye ili asije akaharibu.

Queen Bey aliongoza kwa kuchukuwa tuzo nane katika vipengele 11 alivyokuwa amewekwa kwenye tuzo hizo.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents