Michezo
Video: Payet azidi kuonesha uwezo wa kupiga faulo ligi ya Ufaransa
Dimitri Payet ameendelea kuonesha uwezo wake wa kupiga faulo wakati akiiongoza timu yake mpya ya Olympique Marseille iliyoshinda magoli 2-0 Jumatano hii dhidi ya Guingamp kwenye muendelezo wa ligi kuu ya Ufaransa.
https://youtu.be/RDa_57vW2z0
Magoli ya Marseille yalifungwa na Bafetimbi Gomis kwenye dakika ya 26 na Payet dakika ya 76.
Wakati huo huo mchezaji wa zamani wa Manchester United, Mephis Depay alifanikiwa kuifungia timu yake ya Olympique Lyonnais goli la kwanza wakati wakishinda magoli 4-0 dhidi ya Nancy.