Burudani
Video: Msikilize T-Pain anapoikacha Auto-Tune, utapenda sauti yake?
Pamoja na kwamba T-Pain hakuwa msanii wa kwanza kutumia Auto-Tune kwenye nyimbo zake, kwa wengi anatambulika kama muasisi.
Yeye kwa upande wake aligundua Auto-Tune kwenye remix ya wimbo wa Jennifer Lopez.
Muimbaji huyo ambaye jina lake halisi ni Faheem Rasheed Najm amekubali challenge ya kuimba nyimbo bila Auto-Tune. Na kwenye video hiyo juu, T-Pain anaimba nyimbo tatu live.