Burudani
Video mpya ya Diamond ‘Ntampata Wapi’ imevuka views laki moja Youtube ndani ya saa 24
Video mpya ya Diamond platnumz ‘Ntampata wapi’ imekuwa na mapokeo mazuri kiasi cha kuwavutia watu wengi kutaka kuitazama kila wanaposikia kuwa imetoka.
Video hiyo iliyoanza kuchezwa na vitu vikubwa vya nje kikiwemo MTV Base juzi kabla haijasambazwa kwenye vituo vya hapa nyumbani jana, mpaka sasa imefanikiwa kupata views 116,967 kwenye mtandao wa Youtube, ikiwa ni ndani ya saa 24 toka ipandishwe kwenye mtandao huo.