Burudani
Video: Hush Up The Silence ya Wizkid yawachanganya Pogba na Lingard
Ni ukweli usiopingika kwa sasa Wizkid hana mpinzani Afrika kutokana na muziki wake kufika mbali zaidi. Wimbo wake mpya wa ‘Hush Up The Silence’ aliomshirikisha Drake umeonekana kukubalika na wachezaji wa Manchester United akiwemo Poul Pogba, Jesse Lingard na Fosu-Mensah.
https://youtu.be/M-rDXB0s0Yc
Wachezaji hao ambao ni marafiki wa karibu zaidi wameonekana katika kipande cha video ambacho Pogba amekiweka katika mtandao wa Instagram akicheza na Lingard wimbo huo kwa staili zao bianafsi huku Mensah akirekodi video hiyo.
Baada ya kuweka video hiyo, Pogba kupitia mtandao huo aliandika, “Having fun with my bro new celebration ????????????@jesselingard@tfosumensah51 #happy #blessed #pp.”