Mchezaji kutoka Malaysia Mohd Faiz Subri ameshinda tuzo ya Puskas inayotolewa na FIFA kwa mfungaji wa bao bora zaidi wa mwaka.
Faiz akikabidhiwa tuzo yake na Ronaldo
Faiz, ambaye anayechezea klabu ya Penang FA ndiye raia wa kwanza kabisa wa Malaysia kuwa mshindi wa tuzo hiyo.
Mchezaji ambaye ana miaka 29, alipata karibu asilimia 60 ya kura zilizopigwa kwa bao lake la frikiki alilofunga katika mechi ya Ligi Kuu ya Maaysia dhidi ya timu ya Pahang mwezi Februari
Alikabidhiwa tuzo hiyo na mchezaji soka mahiri kutoka Brazil, Ronaldo.
Hili ndio goli bora la FIFA