Burudani

Lady Jaydee awashukuru mashabiki baada ya kushinda tuzo ya AFRIMMA, Marekani

Lady Jaydee na Diamond July 27 walitangazwa kuwa washindi katika tuzo za AFRIMMA 2014 nchini Marekani.

Lady Jaydee

Diamond alishinda kipengele cha mwanamuziki bora wa kiume Afrika mashariki, huku Lady Jaydee alishinda kipengele cha mwanamuziki bora wa kike Afrika mashariki. Tuzo hizo ziliwashindanisha wanamuziki mbalimbali wakubwa wa Afrika wakiwemo Davido, Mafikizolo, Tiwa Savage, Fally Ipupa, Flavour na wengine.

Lady Jaydee kupitia ukurasa wake wa Facebook aliwashukuru mashabiki wake, aliandika:

“Nashukuru wote mnaokubali kazi zangu, wote mnaosimama na kutetea JayDee bila kusita, nashukuru kwa Tuzo nyingine tena toka AFRIMMA . Wahenga walinena kuwa utavuna ulichopanda, mapenzi tele kwa kila mtu”

jide afrimma

Katika post nyingine Jide amepost picha ya tuzo yake na kuandika:

“Tuzo yangu ya 30. Asanteni kwa ushirikiano, nimeipokea na ninarudi nayo nyumbani. Shhhhhh! !!! Kimya Kimya”.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents