Burudani
Video: August Alsina azimia na kuanguka jukwaani akitumbuiza
Muimbaji wa R&B anayetamba kwa sasa, August Alsina alijikuta akipata vifafa vya hapa na pale baada ya kuanguka wakati akitumbuiza jukwaani saa 24 zilizopita. Bado ameendelea kulazwa hospitali.
Mwakilishi wa msanii huyo ameuambia mtandao wa TMZ kuwa msanii huyo amelazwa kwenye wodi ya wagonjwa mahututi jijini New York na anapewa matibabu ya kifafa. Alsina alizimia na kuanguka wakati akitumbuiza usiku wa jana jijini humo.
https://www.youtube.com/watch?v=IQaZGp62HaA
Amesema madaktari hawakukuta dawa zozote kwenye mwili wake zaidi ya bangi kwenye mfumo wake. Wanaamini kuzimia kwake kulitokana na kuchoka na kukosa maji.