Burudani
Video: AKA ataja mambo anayohitaji akiwa kwenye tour, promota utamweza?
Umeshawahi kujiuliza inakuaje unapokuwa tajiri na mwenye fedha? Kwa AKA mahitaji anayotaka pindi promota anampomtaka kwenye show si haba.
Kwenye interview na DJ Sabby kwenye kipindi cha The Best Life TV, AKA aliweka wazi kile anachohitaji.
1. AKA anapanda business class pekee
2. Anapanda na ndege za South African Airways tu, hakuna Mango na Kulula.
3. Anataka achukuliwe na SUV
4. Yeye na timu yake huchagua hoteli wanayotaka kukaa
5. Ni lazima awe na mabaunsa watatu hadi wanne kwenye show yake
6. Anahitaji, Redbull, maji, chai ya ginger na taulo
Tazama interview nzima hapo chini.