Burudani
Victoria Kimani kuzindua album yake ‘Safari’ Nairobi, Lagos, J’Burg na pengine Dar
Baada ya kuachia single yake ya kwanza ya Kiswahili na ya kwanza kutoka album yake ijayo, Safari, Victoria Kimani amedai kuwa uzinduzi wa album hiyo utafanyika katika nchi takriban tatu.
Akiongea na kipindi cha Mdundo Bando cha Lake FM ya Mwanza kinachoendeshwa na Kattieh, Kimani alisema kuwa Safari itatoka kabla ya mwaka kuisha.
Alisema uzinduzi wa album hiyo utafanyika Nairobi, Kenya, Lagos, Nigeria, Johannesburg, Afrika Kusini na pengine hata Dar es Salaam, Tanzania.
Album hiyo itatoka chini ya label yake Chocolate City yenye makao yake makuu Lagos.
Msikilize zaidi hapo chini.