Burudani
Vanessa Mdee: Wimbo wangu ujao ni wa rap
Vanessa Mdee amesema hachagui muziki wa kufanya na kwamba kama mambo yakienda alivyopanga, wimbo wake ujao utakuwa wa hip hop (hatuna uhakika kama alizungumza kwa utani ama ni kweli atafanya hivyo).
Akiongea kwenye kipindi cha Power Jams cha East Africa Radio, Jumanne hii wakati akitambulisha wimbo wake mpya ‘Siri’ alioshirikiana na Barnaba, Vanessa alidai kuwa yeye ni mpokeaji wa nyimbo nzuri bila kujali ni wa aina gani.
“Napenda kuonyesha kipaji changu na napenda kufanya vitu vingi sio kwamba nasema nahama. Mimi ni mpokeaji wa muziki mzuri. Nasikiliza reggae, rap, zouk, rhumba, taarab,” alisema Vanessa.