Burudani

Vanessa Mdee adai wazo la wimbo ‘Cash Madame’ amelipata baada ya kuzinguliwa na promota

Msanii wa kike wa muziki, Vanessa Mdee amedai wazo la kuandika wimbo ‘Cash Madame’ alilipata baada ya kuzinguliwa malipo yake ya show ya promota.
vanessa-8

Akiongea katika kipindi cha Mji Wa Burudani cha Choice FM wiki hii, Vanessa alisema “Promota alinizingua kwenye malipo hapo ndipo nilipopata wazo la kuandika wimbo wangu wa Cash Madame,”.

Pia muimbaji huyo amesema kwasasa ajipanga kufanya muziki mzuri zaidi huku akidai wakati wake wa kuwa na familia bado.

Katika hatua nyingine alisema ingawa amesomea sheria lakini kitu ambacho ameamua kukifanya katika maisha yake ni muziki.

“Ni kweli nimesomea sheria ila sijawahi kufanya kazi ya sheria na sio kwamba nilikuwa napenda sheria napenda muziki,” alisema Vanessa Mdee.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents