Michezo

Uwanja wa ndege wa Madeira wapewa jina la Cristiano Ronaldo

Mchezaji wa klabu ya Real Madrid Ronaldo ambaye anaumri wa miaka 32, aliongoza taifa lake kushindwa ubingwa wa Ulaya mwaka jana.

Ronaldo ambaye alizaliwa katika mji mkuu wa Madeira, Funchal na baadaye akachezea Sporting Lisbon na Manchester United.


Ronaldo akizindua uwanja wa ndege ambao umepewa jina lake

Uwanja wa ndege wa Madeira sasa umepewa jina la Cristiano Ronaldo.

Baadhi ya wanasiasa wa eneo hilo wamepinga uamuzi wa kubadilisha jina la uwanja wa ndege wa Madeira kuwa Uwanja wa Ndege wa Cristiano Ronaldo.

“Wakati mwingine, shukrani za taifa huwa hazidumu sana, lakini Madeira haitasahau,” Miguel Albuquerque, rais wa serikali ya Madeira alitangaza, hatua ya kubadilisha jina la uwanja huo ilipotangazwa.

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents