Usiku wa Mtanzania
Lady Jay Dee, Sikinde Ngoma , vikundi vya ngoma za asili , Ngoma ya Ukae na Waane Star pamoja na mwanamuziki kutoka Kenya Kidumu wanatarajia kutumbuiza katika sherehe za kuadhimisha kutimiza kwa miaka 10 ya Usiku wa Mtanzania , utakaofanyika katika ukumbi wa Karamjee tarehe 3 Desemba mwaka huu jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi mwendeshaji wa Hoteli ya Peacock Damas Mfugale aliwaambia waandishi wa habari leo kuwa Peacock hoteli ni hoteli inayodumisha na kuendeleza mila, desturi na utamaduni wa mtanzania , hivyo kwa kuwajali wateja wakaanzisha usiku wa mtanzania ambapo vyakula vya asili ya Tanzania vinaandaliwa kwa ladha ya asilia.
Sherehe hii itaadhimisha kutimiza kwa miaka 10 ya usiku wa Mtanzania ambapo kila siku ya Jumatano huwa ni desturi ya kuwa na usiku wa mtanzania na manthari ya hoteli hugeuka na kuwa ya asili ili kuleta maana halisi ya lengo la usiku huo.
Pia katika usiku wa Mtanzania wa kutimiza miaka kumi Benki ya Posta, Shear Illusions, Vayle Springs, na Precision Air ni makampuni ambayo yamedhihirisha kuunga mkono mila na desturi za kitanzania.