Burudani
Umeshawahi kufikiria kolabo ya Dogo Janja na Ben Pol?
Umeshawahi kufikiria kuhusu kolabo ya Ben Pol na Dogo Janja? Sasa fikiria itakuwaje endapo ikitokea.
Kupitia kipindi cha FNL cha EATV, wawili hao wamethibitisha kuwa tayari wameshawahi kufanya klabo ambayo bado haijatoka.
“Tumeshawahi kufanya kazi pale kwa Emma The Boy lakini bado haijatoka. Kuna dude letu lipo ndichi linapumua tu,” amesema Dogo Janja.
Kwa sasa Ben Pol ameachia video ya wimbo wake mpya ‘Phone’ ambao amemshirikisha Mr Eazi.