Ujio mpya wa Mzee Chilo, Uwoya na Haji Adam
Jana nilikuwa nimepozi wakati nikiangalia uchukuaji wa Movie moja ambayo ilivutia sana kutokana na Scene zake kuwa za kuvutia. Yote zaidi ya yote nilivutiwa sana na mwigizaji Irene Uwoya, ambaye mara kwanza nilikuwa nikidhani kwamba huenda aliingia kwenye sanaa kwa bahati mbaya, bila kujua uwezo alio nao. Jana nikagundua Uwoya ambaye aliigiza kama Polisi aliweza kunikuna sana kutokana na uhusika jinsi alivyouvaa na kunifanya nisisimke na kuvutia hasa na hiyo filamu hata kabla haijaisha na kuingia mtaani
Zaidi ya Irene Uwoya, pia nilivutiwa na Swahiba wangu wa karibu Haji Adamu, maarufu kama mkali wa hisia hasa pale alipokuwa akitoa hisia zake, akitamani kulia. Jb ndiye aliyekuwa Director wa filamu hiyo, wakati mzee Chilo akiingiza kama mkuuwa polisi. Hebu angali baadhi ya scene na utani ambao ulikuwa ukifanyika wakati wa uandaaji wa filamu hii.