Bongo Movie
Uigizaji wamzuia Aunt Ezekiel kukaa na mumewe Dubai
Muigizaji wa filamu nchini, Aunt Ezekiel amesema kilichomfanya ashindwe kukaa Dubai na mume wake ni kazi ya uigizaji ambayo anaitegemea na hataki ipotee maishani mwake.
Akiongea na Bongo5 leo, Aunt amesema kutokana na kazi yake kubwa anayoitegemea katika maisha yake ya kuigiza filamu, na soko lake lipo Tanzania itamwia vigumu kukaa Dubai kwa mumewe.
Hata hivyo ameongeza kuwa atakuwa anafanya kazi zake za filamu hapa nchini na kurudi Dubai kwa mume wake.
“Sasa nikisema nikae Dubai muda wote ni lazima kipaji changu kitapotea, hivyo nafanya kazi zangu kwa kutengeneza filamu kama tatu, kisha narudi Dubai kidogo kukaa na mume wangu,” Alisema Aunt.