Burudani
Ubabaishaji umekithiri baada ya muziki kuwa dili – Mwana FA
Msanii wa muziki wa Hip Hop, Mwana FA amesema aliandika wimbo ‘Asanteni Kwa Kuja’ ili kuwapa ujumbe wasanii wasio na vipaji kwamba muda wao umeisha.
Akizungumza katika kipindi cha Jahazi cha Clouds FM, Mwana FA alisema wasanii wengi wasio na vipaji waliingia kwenye muziki baada ya kuona unalipa.
“Wasanii wengi waliingia kwenye game bila sababu sahihi, kwahiyo kuna ujanja ujanja mwingi, ubabaishaji umekithiri baada ya muziki kuwa dili. Kwahiyo kuna uongo uongo mwingi. kwahiyo ni kama tunawashukuru kwa kuja na tunawaambia hapa shughuli ipo, muda wao umeisha, ndio maana kuna ile verse ‘Here comes the beat, here comes the beast, Mother, I’m still the best’.” Alisema FA