Tyson Fury: Amshangaa Klitschko kwa kujiruhusu kupigwa na ‘manyama uzembe’ kama yeye
Bondia kutoka nchini England, Tyson Fury haishi vituko amevua fulana yake kuonyesha kitambi huku akimkandia mpinzani wake, Wladimir Klitschko kwa kujiruhusu kupigwa na ‘manyama uzembe’ kama yeye.
Alifanya kituko hicho katika Mkutano na Waandishi wa Habari kuelekea pambano lao la marudiano la uzito wa juu litakalofanyika baadae mwaka huu kwanza kaingia na warembo ambao kwenye makalio kuna herufi zinazounda jina lake.
Fury ambaye atatetea mataji yake ya dunia ya WBA na WBO aliyoyatwaa kwa kumshinda Klitschko mjini Dusseldorf, Ujerumani Novemba mwaka jana katika pambano litakalofanyika ukumbi wa Manchester Arena Julai 9.
Kama haitoshi, akaanza kumshangaa Klitschko kushindwa na mtu kama yeye ambaye alijiita bonge. Akavua shati na kuonyesha tumbo lake.
Tyson aliendelea kuendelea kusisitiza kushangazwa na mpinzani wake asiyeweza kuonyesha uwezo wake na kumshinda bonge kama yeye.