Burudani
Tyga apanga kumchukua mwanae kutoka kwa Blac Chyna akidai mama yake anakula bata 24/7
Tyga anadhani Blac Chyna hana uwezo wa kumlea vyema mwanae sababu muda mwingi amekuwa akijirusha na kula bata.
Rapper huyo ana wasiwasi kuwa Blac Chyna anavutiwa zaidi kwenda club kuliko kumlea mtoto wao mwenye miaka 2 King Cairo, na sasa amepanga kuiomba mahakama impe ruhusa ya kuishi naye.
Tyga anaamini mzazi mwenzie amepoteza focus ya kumlea mtoto wao kwakuwa anaendekeza kutwerk na kuuza nyago. Alichukia zaidi pale alipoona Blac Chyna na Amber Rose wakitwerk.
https://www.youtube.com/watch?v=0v9FQobkW1w
Pia hataki mtoto wake alelewe na wafanyakazi wa ndani.
Wapenzi hao wa zamani hawana amri ya mahakama ya nani anatakiwa akae na mtoto lakini mara nyingi mtoto amekuwa akikaa na mama yake.